b..

B1

Wynem

animation

Thursday, March 27, 2014

BATULI WA BONGO MUVI AFUNGUKA, WANOFANYA UFUSKA BONGO MUVI WANATUHARIBIA

Msanii wa filamu za Kibongo, Yobnesh Yusuph  ‘Batuli’.

MSANII wa filamu za Kibongo, Yobnesh Yusuph  ‘Batuli’ amesema tabia mbaya za baadhi ya wasanii wenzao ndizo zinazowaharibia na kuwafanya wote waonekane hawana maadili.

Akiteta na safu hii, Batuli alisema amekuwa akipata malalamiko kuwa hawatumii katika filamu zake za watoto Jenifer na Jamila waliokuwa wakifanya kazi na marehemu Steven Kanumba, jambo ambalo amelikanusha.

“Siwezi kuwanyima watoto nafasi ya kuonyesha vipaji vyao, sema watu hawajui kilichopo nyuma ya pazia. Nimeshawahi kuwaita lakini wazazi wao wakawazuia kwa madai siku hizi bongo muvi ni ufuska tu na hakuna kazi kama zamani. Ilibidi nimchukue yule mtoto mwingine mvulana Patrick.

“Fikiri nafasi ya msichana inalazimishwa hadi anacheza mvulana ni tatizo. Wasichokijua watu ni kwamba, wazazi wao wanawazuia wakiogopa wataharibika. Wasanii tubadilikeni jamani,” alisema Batuli.

Chanzo: Kandili yetu blog.  

No comments:

Post a Comment