b..

B1

Wynem

animation

Tuesday, June 23, 2015

ILIVYOKUWA KWENYE ZIARA YA JANUARY MAKAMBA MKOANI SHINYANGA.

Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akisalimiana na kuzungumza jambo na mmoja wa wananchama wa CCM Mkoa wa Shinyanga alijitokeza kumdhamini. Ambapo mkoani Sinyanga amejizolea wadhamini 6228 ikiwa ni idadi ya Shinyanga Mjini na Wilaya ya Shinyanga Vijijini.
Mh January Makamba akihutubia wananchi na wanachama wa CCM mkoa wa Shinyanga waliojitokeza katika Viwanja vya CCM Wilaya wa Shinyanga Mjini. January yupo katika ziara yake ya kusaka wadhamini ndani ya chama ambao watamuwezesha kuteuliwa kuwania nafasi ya urais wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM. Ambapo mkoani Sinyanga amejizolea wadhamini 6228 ikiwa ni idadi ya Shinyanga Mjini na Wilaya ya Shinyanga Vijijini.
Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akionesha fomu ya udhamini iliyowekwa sahihi na na wanachama 6228 mara baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na katibu wa wilaya ya Shinyanga mjini.
Mbunge wa Shinyanga Mjini Steven Masele azungumza na wananchi pamoja na wanachama wa CCM mkoa wa Shinyanga na kumkaribisha Mh January Makamba kuzungumza na wananchi hao waliojitokeza katika viwanja vya ofisi ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akiteta jambo na mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Masele walipokuwa katika mkutano na wananchi pamoja na wanachama wa CCM mkoani Shinyanga. Mkutano huo ulifanyika katika viwanja vya CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mh. January Makamba akiweka sahihi kwenye vitabu vya wageni katika ofisi za CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini.
Mh anuary Makamba akiwapungia mkono wananchi na wanachama wa CCM nje ya Ofisi ya Chama hicho wilayaya Shinyanga Mjini mara alipowasili kwa ajili ya kuomba udhamini kutoka kwa wanachama hao utakaomuwezesha kupata ridhaa ya chama kugombea nafasi ya urais wa Tanzania.
Baadhi ya waendesha Bodaboda waliojitokeza kumpokea Mh January Makambawakiwa kwenye msafara wa kuelekea katika viwanja vya CCM wilaya ya Shinyanga Mjini. Ambapo mkoani Sinyanga amejizolea wadhamini 6228 ikiwa ni idadi ya Shinyanga Mjini na Wilaya ya Shinyanga Vijijini. Picha zote na Mpiga Picha wetu.

No comments:

Post a Comment