b..

B1

Wynem

animation

Thursday, June 25, 2015

MR. BLUE AIPA KISOGO MIHADARATI

Anaitwa Khery Sameer aka Lil Sama...wengi tunamjua kwa jina la Mr.Blue ingawa jina hili hakujipa yeye,Ni jina lililozaliwa baada ya single yake ya Blue Blue kufanya vizuri na watu kuamua kumpachika jina hilo.
Wakati anatoka alikua akishindanishwa na Joselin mkali mwingine ambaye style yao ya kuchana ilikua ikiwachanganya mashabiki wengi mpaka @princedullysykes alipoamua kuwaweka pamoja kwenye wimbo wa DHAHABU.
Zaidi ya miaka 12 Blue amedhihirisha ukali wake kwa kuwaacha mbali watu aliokuwa akishirikiana nao kwa kipindi kile akiwemo Abbyskils.
Blue ni miongoni mwa wasanii wachache wenye bahati ya kuliteka jukwaa hata bila ya kuwa na single mpya na mashabiki wakampokea na kumshangilia,ana mfululizo wa single kadhaa zilizompa mafanikio ikiwemo single ya PESA aliyoitoa mwaka 2013.
Leo tunamsherehekea kwa maamuzi mazito aliyoamua kuyatangaza na kuyaweka wazi wiki chache zilizopita maamuzi ya kuamua kuacha kutumia Mihadarati yote aliyowahi kutumia kipindi cha nyuma.
Blue ameishukuru Familia yake ambayo ni mkewe na mtoto wake kwa nguvu yao kubwa iliyosababisha aache kutumia vilevi hivyo.
Hiko ni kwa uchache kutoka kwa super star wetu wa Tanzania @mrbluebyser1988 @mrbluebyser1988 ipi sifa nyingine ya Blue unayoifahamu?? #‎kuzamuzikitanzania #kuzamuzikitanzania c


No comments:

Post a Comment